Mbeto awataka wana CCM kujivunia rasilimali watu wake


Na Mwandishi  Wetu , Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi  kimesema CCM ni taasisi kubwa imara  yenye wanachama  wengi wenye uwezo na fani tofauti hivyo  Mwenyekiti  wake hapaangiwi yupi wakufanya kazi naye kwa wakati  upi na lini.


Aidha,CCM kimesisitiza kuwa kutokana na taasisi hiyo kuwa kubwa na tegemeo kwa  Taifa,itaendesha kazi zake bila kupangiwa au kwa shindikizo.


Hayo yametamkwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Idara  ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis aliyesema CCM kina hazina kubwa  isiofilisika ya Viongozi wa chama na Jumuiya  zake.


Mbeto alisema  kila Mwanachama wa CCM mwenye  uwezo, upeo na maarifa  ya utendaji  kazi za kisiasa, hupata nafasi kwa  muda  na wakati  wake.


Alisema ndani  ya CCM  na kwenye  Serikali zinazoongozwa na chama hicho ,kuna kazi nyingi ambazo zinawahitaji wanachama wenye uzalendo, nidhamu, utii na uvumilivu. 


"Mwenyekiti  wetu  hapangiwi yupi au nani afanye naye kazi lini  au  kwa wakati  gani na yupi anaetosha. Kwetu CCM  kila mmoja  ana hadhi na kufaa "Alisema Mbeto.


Aliwataka wanachama wa CCM kuwa watulivu, wenye staha, subira na maadili  bila  pupa au kiherehere. 


"Kuna kazi nyingi.Tuko watu  wengi na wote  tunafaa kukifanyia kazi chama chetu. Hayupo yeyote  peke yake ambaye ni bora zaidi  ya mwingine"Alieleza.


Mbeto alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa kufuatia  video ya mwana CCM  mmoja, kutaka Mbeto akafanye kazi Tanzania  Bara. 


"Wapo watu hawakutegemea kama ningekuwa Mwenezi  wa CCM  Zanzibar. Hata mimi sikukuwa na ndoto  ya kushika nafasi  hii. Wakati  ndio ulioamua na wakati  mwingine unaweza kuamua vinginevyo  "Alisema Mwenezi  huyo

Mbeto awataka wana CCM kujivunia rasilimali watu wake Mbeto  awataka wana CCM kujivunia rasilimali watu wake Reviewed by Gude Media on 12:01:00 PM Rating: 5

No comments

Note: Only a member of this blog may post a comment.