Jumuiya ya Wazazi Temeke yawekwa mguu sawa


Na WANDISHI WETU

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi  ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM)  Wilaya ya Temeke, Hamis Slim, amewakata  viongozi  wa  mabaraza, kamati za utekelezaji za kata na matawi  za jumuiya hiyo kuvunja makundi  yaliyotokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 , 2029 na kufanyakazi kwa ushirikiano.

Ameyasema hayo  Dar es Salaam, leo katika ziara ya Kamati ya Utekelezaji ya  jumuiya hiyo Wilaya ya Temeke, katika Kata za Kiburugwa na Kibondemaji inayo lenga kuwashukuru   wanachama wa jumuiya hiyo kwa ushindi mkubwa wa  CCM na kuimarisha uhai wa jumuiya.

Slim, amesema  uchaguzi umekwisha  hivyo ni wakati muafaka wa kuvunja makundi, kusameheana, kupendana na  kuhudumia jumuiya kwa  ufanisi na weledi.

“Tunawapongeza  Jumuiya ya Wazazi mmeafanya kazi nzuri  katika uchaguzi mkuu na kuipatia  ushindi wa kishindo  CCM na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Sasa ni wakati wa kuleta maendeleo. Tuzike tofauti zetu zilizotokana na uchaguzi. Mwiba ulipoingia ndipo unapotokea,”amesema.