Vikundi zaidi ya 100 kupata mafunzo ya uchumi na ubunifu Dar


Na MWANDISHI WETU

ZAIDI ya  vikundi 100  vya wajasiriamali wanawake  kutoka  Mkoa wa Dar es salaam, vinatarajia   kupata mafunzo ya uwezeshaaji kiuchumi, kuongeza uelewa na ubunifu.


Hayo yamesemwa na  Mbunge wa Viti Maalumu , Amina Good Said, ambaye ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Amo Foundation, jana.


Amina amesema  mafunzo hayo yatafanyika  Februari  13 mwaka huu, wilayani Ilala jijini Dar es Salaam.


“Tutayafanya katika  Ukumbi wa Blessing uliopo  katika Kata ya  Segerea. Vikundi zaidi ya 100 vitapata mafunzo hayo bila malipo,”amesema.


Amina ameeleza  mafunzo hayo yatafunguliwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Halima Mamuya.


“Ni mafunzo muhimu yatakayo walenga wanawake na makundi yote ya kinamama yanayofanya shughuli za kiuchumi. Tunataka kuwajengea uelewa  katika masuala mbalimbali  ya kiuchumi na ubunifu wa  shughuli zao,”amesema Amina.


Amebainisha  dhamira  ni  kuwasaidia wanawake hao  kujiongezea kipato  na masoko  ya uhakika ya bidhaa zao.

Vikundi zaidi ya 100 kupata mafunzo ya uchumi na ubunifu Dar Vikundi zaidi ya 100 kupata mafunzo ya uchumi na ubunifu Dar Reviewed by Gude Media on 4:36:00 AM Rating: 5

No comments

Note: Only a member of this blog may post a comment.