TASAF yajivunia kufikia malengo kwa kaya maskini


 Na MWANDISHI WETU


Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Zanzibar, umesema umefanikiwa

malengo yake kwa kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo ya kila siku,

zikiwemo katika sekta ya elimu, afya, maji na kuzisimamia kaya zao.


Akizungumzia kuhusu mafanikio ya mpango wa kunusuru kaya masikini

Zanzibar, Mratibu wa Tasaf Zanzibar, Makame Ali Haji, alisema mpango

huo umetekelezwa kwa vipindi vinne kwa mafanikio makubwa.


Alisema Tasaf imetekeleza katika usambaji wa fedha, miradi ya ujenzi

katika maeneo yenye uhitaji, utekelezaji wa miradi ya ajira za muda na

kukuza uchumi wa kaya na kuweka akiba.


Makame alisema kuhusu usambazaji wa fedha kwa upande wa Zanzibar,

zaidi ya kaya 54,425 zimewezeshwa na zaidi ya Sh, bilioni 52

zimetumika.


"Fedha hizo zimewawezesha wananchi kuanzisha miradi midogo midogo ya

kuzisaidia kaya zao na kuhakikisha wanakuza vipato vyao, makazi yao

pamoja na kuendelea maisha yao", amesema.


Kupitia utekelezaji wa ajira za muda, Tasaf imetekeleza  zaidi ya

miradi 711 kwa upande wa Unguja na Pemba, katika sekta ya misitu,

maji, afya, elimu na ukarabati wa barabara za ndani ili wananchi

wapate huduma kukuza uchumi wa kaya zao.


"Miradi hii 711 imesaidia sana kutatua  changamoto mbalimbali kaya na

kuwainua kiuchumi wananchi kwa ujumla", amesema.


Kipengele cha ujenzi wa miundombinu, Makame alisema Tasaf kupitia

miradi katika sekta ya afya na elimu, ambapo zaidi ya Sh. bilioni 4,

zimetumika  katika sekta hizo.


Makame amesema kupitia mpango wa Tasaf wametekeleza ujenzi wa

madarasa, ukarabati wa barabara na ujenzi wa vituo vya afya katika

maeneo yenye uhitaji.


Kupitia miradi ya uwezeshaji jamii kiuchumi, Makame amesema baada wa

wanufaika kupatiwa fedha kupitia usambazaji, kuna ruzuku maalumu

zimetolewa kwa kaya 24,435 Unguja na Pemba.


Amesema katika utekelezaji huo zaidi ya Sh. bilioni 9.4 zimetmika

kuwawezesha kupitia miradi midogo midogo, ikiwemo kuanzisha miradi ya

ufugaji, kilimo, biashara ndogo na huduma, ambapo wananchi wengi

wamepiga hatua na kupelekea kutoa ajira kwa wengine.


"Mengi yamefanyika katika muungano huu ambao umefika miaka 61,

naishukuru serikali na wananchi kwa kuhakikisha kila kinachopangwa

kinafikia  malengo, ambapo mpango wa kunusuru kaya masikini

umefanikiwa", amesema.


Kwa upande wa wanufaika wa TASAF wamesema mpango huo umewasaidia

kutimiza ndoto zao katika sekta ya elimu, ujasiriamali na kuwainua

kiuchumi.


Mwanafunzi wa Chuo cha Abdulrahman Al-Sumaiti, Miraji Alfani Musa,

amesema TASAF imekujua kuinua familia za watu wa chini, imemsaidia

tangu akiwa kidato cha nne hadi sasa kupitia kwa wanufaika wazazi

wake.


"Nimepata mkopo wa elimu ya juu kutoka Bodi ya Mikopo, kwa msaada

TASAF nilipewa kipaumbele, hivyo naishukuru serikali kwa kuwa na

mpango huu muhimu kwa wenye kuhitaji, naomba Tasaf iwe endelevu",

amesema.


Naye mwanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar (SUZA), Mtumwa Ali Haji,

amesema alifurahi kufaulu kwa kupata ufaulu wa daraja la pili kidato

cha nne, lakini wazazi wake walimwambia hawana uwezo wa kumuendeleza

ndipo alikata tamaa ya kutimiza ndoto  zake.


Mtumwa amesema furaha yake ilirejea baada wazazi kufikiwa kwa kujiunga

mpango wa TASAF, ambapo alipatiwa mkopo wa elimu kutoka bodi ya mikopo

na kuendela na masomo, ambapo anasoma Shahada ya Manzingira kataika

chuo hicho.


"TASAF ndoto yangu ni kuwa waziri wa mazingira, sasa matumaini hii

ndoto itatimia kupitia fursa hii Tasaf", mesema.


Mkazi wa Kiembe Samaki, Hamid Juma Sheha, amesema alikuwa katika

mpango huo, alianza kulipwa kidogo kidogo baada muda akupita alipewa

fedha nyingi, akaamua kuanzisha miradi mbalimbali ya kumuendeleza.


"Nilipopata fungu kubwa Sh. 450,000 kutoka TASAF nikaanza kukusanya

malighafi na kumchukua kijana wa kunisaidia katika kazi yangu ya

kutengeneza chaga za udogo za kutengeneza majiko, baada kupata faida

nikaanzisha mradi mwingine wa kuku, nilianza na kuku 100 na sasa nina

kuku 300", amesema.


Hamid amesema kupitia TASAF amefanikiwa kupata fedha kusomesha watoto

wake wawili katika ngzi chuo na wengine wawili wako kataika shule za

msingi.


Pia Hamid ameshukuru mpango huo kwa kumuinua kiuchumi, amewashauri

wanufaika wengine kujifunza kwake kwa kutumia fedha wanazopewa

kuanzisha miradi kuliko yote kuingiza katika matumizi tofauti.





TASAF yajivunia kufikia malengo kwa kaya maskini TASAF yajivunia kufikia malengo kwa kaya maskini Reviewed by Gude Media on 9:58:00 AM Rating: 5

No comments

Note: Only a member of this blog may post a comment.