Na MWANDISHI WETU, Dar es Salaam
Shirikisho
la Taasisi za Hijja Tanzania Bara (TAHAFE) limeandaa Kongamano na Maonesho ya
Hajj 2027 na kuzitaka taasisi za hijja
na mahujaji watarajiwa kukamilisha malipo ya maandalizi kwa wakati, kuepusha
changamoto zinazotokana na ratiba mpya zilizowekwa na mamlaka za Saudi Arabia.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Dar es Salaam, Julai 15, Naibu Katibu wa TAHAFE, Mahamed Mshangama, amesema kongamano hilo litafanyika Agosti 15, 2027 katika Ukumbi wa Lamada, Ilala, kwa lengo la kutoa elimu, mwongozo na kuonesha huduma zinazotolewa kwa mahujaji kupitia taasisi za hijja nchini Tanzania na Saudi Arabia.
Mshangama
amesema kutokana na mabadiliko ya ratiba ya Wizara ya Hajj ya nchini Saudi
Arabia, taasisi zote zinazosimamia mahujaji zinapaswa kuhakikisha zinakamilisha
malipo ya gharama za maeneo ya malazi na mahema kabla ya Agosti 13, 2026, ambao
ni mwisho wa muda uliowekwa na mamlaka za nchi hiyo.
Pia Mshangama amezitaja taasisi na mawakala walioidhinishwa kusafirisha mahujaji wa Tanzania Bara kwa mwaka 2027 kupitia mwavuli wa BITHA Bara na TAHAFE, ili kwalinda na matapeli.
Taasisi hizo
ni Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Jamarat, Travel, Al Husna, Hajj Trust,
ZamZam, Rawdhwa, Masjid Adil, Kidunda,
Ajwah, M2, Manasik, Musafir, Ahlubait, Nurpath.


