Selwa amewataka wasimamizi wa mafundi na Kamati za ujenzi kusimama katika nafasi zao miradi ikamilike kwa wakati



Na MWANDISHI WETU, TABORA

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid amewataka Wasimamizi wa Mafundi na Kamati za ujenzi kusimama  katika nafasi zao kwa lengo la kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa wakati na kuzingatia viwango vya fedha.

Selwa ametoa wito huo, wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali katika kata za Jimbo la Manonga wilayani Igunga.

"Tujirekebishe kwenye miradi yetu na kuongeza usimamizi kwa sababu hali ya  mafundi kuondoka maeneo ya ujenzi wakati unaendelea  hatukubaliani nayo," amesisitiza na kuongeza kuwa:

"Ziogopeni fedha hizi za miradi kama ukoma na mambo ya udalali yasiwepo kwenye miradi, wapeni mafundi wanaofanya kazi ipasavyo", alisema. 





Selwa amewataka wasimamizi wa mafundi na Kamati za ujenzi kusimama katika nafasi zao miradi ikamilike kwa wakati Selwa amewataka wasimamizi wa mafundi na Kamati za ujenzi kusimama katika nafasi zao miradi ikamilike kwa wakati Reviewed by Gude Media on January 12, 2026 Rating: 5

Boxed Width - True/False

True