Mpogolo: JMAT nendeni mkashughulikie migogoro ya kijamii kuanzia ngazi ya familia, ardhi na changamoto za mirathi



Na MWANDISHI WETU 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo ameitaka Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), kushughulikia changamoto za kijamii kuisaidia Serikali kurudisha furaha na kuleta maridhiano katika ngazi za familia.


Mpogolo amesema hayo Januari 14,2026 katika uzinduzi wa idara tatu mpya za jumuiya hiyo, Karimjee jijini Dar es Salaam.


"Nendeni mkashughulikie migogoro ya kijamii kuanzia ngazi za chini za familia, kashughulikieni changamoto za mirathi, migogoro ya ardhi, migogoro ya ukatili hasa ya unyanyadaji wa kijinsia maana jamii inawahitaji sana" amesema.


Mpogolo amsema JMAT ikafanye kazi za maridhiano kwasababu ni chombo ambacho Serikali kinawategemea kuleta maridhiano, hususan katika ngazi za familia kwakuwa  wanajukumu ya malezi na kutatua changamoto,  kero za kijamii.

 

Pia Mpogolo ameiomba jumuiya isichoke kushirikiana na Serikali kwasababu wananchi wanauhitaji mkubwa katika kusaidiwa kutatua changamoto zao.

 

Aidha ameipongeza JMAT kwa kutoa elimu ya amani nchini, kutatua changamoto za kisiasa na kuleta upatanisho wa dini mbalimbali pindi inapojitokeza migogoro.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Sheikhe Alhad Mussa Salum, amesema watahakikisha taifa linakuwa na amani muda wote kama walivyokabidhiwa kutoka kwa waasisi wa taifa hili likiwa salama na amani.

 

"Hatutakubali amani ya nchi itoweke kirahisi, tutahakikisha migogoro inapojitokeza basi sisi kama Jumuiya tutasimama kurejesha amani hiyo" Alhad Salum.

 

Amesema JMAT wameona waongeze nguvu katika kuongeza idara tatu ikiwemo ya wazee, wanawake na vijana ili kuongeza nguvu katika kazi za marishiano nchini. 





Mpogolo: JMAT nendeni mkashughulikie migogoro ya kijamii kuanzia ngazi ya familia, ardhi na changamoto za mirathi Mpogolo: JMAT nendeni mkashughulikie migogoro ya kijamii kuanzia ngazi ya familia, ardhi na changamoto za mirathi Reviewed by Gude Media on January 15, 2026 Rating: 5

Boxed Width - True/False

True