MPOGOLO: Tutatekeleza agizo la Rais kuhusu maridhiano


 

Na MWANDISHI WETU

Mluu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema wataendelea kutekeleza maelekezo na maagizo ya  falsafa ya  Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  ya maridhiano  kulijenga Jimbo la Segerea na  wilaya hiyo .

Mpogolo Amesema hayo Dar es Salaam, alipozungumza na wenyeviti wa serikali za mitaa 61 ya jimbo hilo.

Mkutano huo umeitishwa  na Mbunge wa  jimbo hilo, Agnesta Kaizer wa Chama cha CHAUMA kuomba ushirikiano wa kiutendaji na wenyeviti hao, ikiwa ni hatua ya  kujenga maridhiano.

Mpogolo amepongeza  hatua ya mbunge huyo,  Agnesta na kuwa hatua hiyo ni kutekeleza maelekezo ya  Rais Dk. Samia na itasaidia kujenga jimbo hilo na  Wilaya ya Ilala.

“Ninyi wenyeviti  mkishirikiana na mbunge na sisi shida za watu tukihangaika nazo, tukaziweka katika listi tukaona namna za kuzitatua moja baada ya nyingine tutakuwa tumegusa na watu.

"Mnambunge anaye gusa watu. Mnyororo wa uongozi unajengwa na uhusiano lakini msingi ni zile shida za watu,”amesema Mpogolo.

Kwa upande  wake Agnesta, alisema lengo la  mkutano huo ni kuwaomba  ushirikiano wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji ambao wote wanatokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Amesema ufanisi wa  wananchi wa Jimbo la Segerea utatokana na ufanisi wa  wake na  watendaji hao.

“Unapokuwa ni mbunge wa jimbo utakuwa  ni mbunge usiyejitambua  kama hutafahamu kwamba lile kundi namba moja unalolihitaji kwa asilimia mia moja ili uweze kutuimikia wananchi  kwa weledi na ufanisi ni hili kundi la serikali za mitaa,”alisema.

Ameeleza, kama  mbunge asipofanya kazi na kundi hilo kwa umoja, upendo  na weledi hawezi kufanikiwa, jimbo halitofanikiwa na wenyeviti hao hawatafanikiwa kwa sababu ya mahitaji, pia ushirikiano wa mbunge kufanikisha shughuli za maendeleo.

“Jambo la pili  ni kuomba uashirikiano wenu, kwa sababu sasa wote tunatumikia wananchi bila kujali tofauti za kisiasa. Mitaa yote 61 inaongozwa na wenyeviti wa serikali za mitaa wa CCM lakini mimi nitawapa ushirikiano kwa asilimia miamoja,”alieleza.




MPOGOLO: Tutatekeleza agizo la Rais kuhusu maridhiano MPOGOLO: Tutatekeleza agizo la Rais kuhusu maridhiano Reviewed by Gude Media on January 06, 2026 Rating: 5

Boxed Width - True/False

True