Waliokopa sh. bilioni 3.2 Mfuko wa Pembejeo wapewa siku 14 kuzirejesha


 Na MWANDISHI WETU

Kampuni ya  Udalali ya Yono Auction  Mart, imetoa siku 14  kwa wananchi , taasisi na vikundi waliokopa  pembejeo na fedha katika Mfuko wa Pembejeo (AGITF)  kulipa madeni yao kabla ya kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufirisiwa mali zao.


Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam, leo Mkurugenzi wa kampuni hiyo Dk. Scholastika Kevela,  amesema  amepewa maelekezo na serikali  kupitia AGITF kuchukua hatua za kuuza mali za wadaiwa hao ambapo katika orodha hiyo kuna vigogo na wafanyabiashara wakubwa nchini.


Dk. Scholastika ameeleza, wadaiwa hao ni zaidi ya 200 ambao walikopa fedha  na pembejeo mfuko huo wakiamini ni fedha za serikali  zinatolewa bure  hivyo  kuto kurejesha.


“Serikali imeniagiza yoyote aliyechukua fedha katika Mfuko wa Pembejeo awe amerejesha ndani ya siku 14. Kama ulikopa uliwekeza nyumba tutauza fedha ya serikali irejeshwe,” amesema.


 Amebainisha kiama hicho kitawakumba  hata waliowadhamini wadaiwa hao  kwani kwa mujibu wa sheria wanapaswa kulipa fedha hizo.


 “Kwa niaba ya Mfuko wa Pembeje kama mdaiwa aliwekeza nyumba itauzwa ama kama aliwekeza gari  kudhamini mkopo vitauzwa ili  fedha ya serikali irejeshwe. Kukaa na fedha  hii ni utovu wa fedha za umma,”amebainisha.


Aidha ameeleza  operesheni ya kuzisaka na kuuza mali za wadaiwa hao itafanyika nchi nzima na katika orodha aliyokabidhiwa na serikali kuna vigogo, wafanyabiashara wakubwa  na program kubwa za kilimo.



Waliokopa sh. bilioni 3.2 Mfuko wa Pembejeo wapewa siku 14 kuzirejesha Waliokopa sh. bilioni 3.2 Mfuko wa Pembejeo wapewa siku 14 kuzirejesha Reviewed by Gude Media on 8:44:00 AM Rating: 5

No comments

Note: Only a member of this blog may post a comment.