Halmashauri ya Igunga imejipanga kuhakikisha wanafunzi wote wanaendelea kufaulu kwa asilimia zote

 


IGUNGA - TABORA 

KUELEKEA muhula mpya wa elimu 2026, viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora wamejipanga vema kuhakikisha Wanafunzi ngazi ya Awali, Msingi na Sekondari wanaendelea kufaulu kwa asilimia 100.


Akizungumza na Watumishi wa Masijala, Maofisa Waendesha Ofisi na  Idara za Elimu Msingi na Sekondari wanaofanya kazi Makao Makuu ya Halmashauri hiyo, Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu ( DAHRO), Hamisi Hamisi amewakumbusha Wakuu wa Idara hizo kuendelea kuwajali Walimu.


Aidha, amewaomba viongozi hao kuendelea kutoa taarifa kwa Mwajiri  kwa wakati  ikiwa kunawalimu ni watoro kazini na kuwafahamu watumishi wanaotarajia kustaafu kwa lengo la kuandaa stahiki zao mapema.


Pia,  amewakumbusha kutenga bajeti ambayo itatumika kutoa mafunzo ya awali kwa walimu ambao wanaajiriwa kwa sababu itawasaidia kuepuka malalamiko, lugha zisizo na staha na kushitaki kwa mwajiri wao mara kwa mara.





Halmashauri ya Igunga imejipanga kuhakikisha wanafunzi wote wanaendelea kufaulu kwa asilimia zote Halmashauri ya Igunga imejipanga kuhakikisha wanafunzi wote wanaendelea kufaulu kwa asilimia zote Reviewed by Gude Media on 5:30:00 AM Rating: 5

No comments

Note: Only a member of this blog may post a comment.