TANGAZO

Tume ya waita wananchi Ilala kutoa maoni matukio Oktoba 29



Tume ya  Uchunguzi wa Matukio   Yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi  Mkuu Oktoba 29,  mwaka 2025 imeanza kusikiliza maoni ya   wananchi  wilayani  Ilala , jijini Dar es  Salaam.


Akizungumza na waandishi wa habari, Mjumbe wa  tume hiyo, Balozi Ombeni Sefue, amewataka wananchi kujitokeza  kutoa maoni yao  kuhusu walicho shuhudia wakati na baada ya matukio  yaliyotokea Oktoba 29, 2025.


Amesema   hiyo ni fursa muhimu  kwa wananchi  na wasisubiri  baada ya tume kumaliza kukusanya maoni ndipo waanze kulalamika.


“Tunataka kila mtu aliyeshuhudia  ajitokeze katika tume. Isije akajitokeza mtu baada ya tume kumaliza kazi yake akaanza kulalamika. Tulipewa siku 90 na Rais (Dk. Samia Suluhu Hassan)  ambazo zitamalizika Februari mwaka huu",  amesema Balozi  Sefue.


Ameeleza tume hiyo  imezunguka katika mikoa mbalimbali nchini na hivi sasa inakusanya maoni katika ngazi za chini za wilaya  ambapo  aliwashukuru wananchi kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao.


“Katika Mkoa wa Dar es Salaam, tume imegawanyika. Wengine wako Temeke na wengine Ilala. Tutakuwa Kinondoni na Ubungo kisha Kigamboni", amesema Sefue.


Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo,  amewahimiza  wananchi kujitokeza kutoa maoni yao mbele ya tume hiyo.


Amewataka   walioathirika , kufiwa na nfugu zao, kujeruhiwa , kuharibiwa  na kuibiwa mali zao kujitokeza.


Tume hiyo inayoongozwa na Jaji  Othuman Chande,  iliundwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kufanya  uchungizi wa matukio  yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka jana hapa nchini.

Post a Comment

0 Comments